Baada ya taarifa kusambaa katika mitandao ya kijamii zikidai kwamba msanii Omary Nyembo maarufu Ommy Dimpoz kuwa amelazwa hospitali katika chumba cha uangalizi maalum (ICU), uongozi wa kampuni imekanusha taarifa hiyo.
Akizungumza na MCL Digital leo Jumamosi Agosti 25, 2018, meneja wa msanii huyo Seven Mosha amesema hali ya msanii huyo kwa sasa inaendelea vizuri.
Amesema Ommy Dimpoz alifanyiwa upasuaji wa koo miezi minne iliyopita na tangu hapo hali yake imekuwa ikiendelea vizuri hadi sasa.